Nenda kwa yaliyomo

Wakia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wakia (kutokana na Kiarabu: وقية - اوقية, awqiyah - waqiyah) unaweza kuhusu maana mbili:

Wakia asilia

Wakia asilia ni kipimo asilia kimojawapo cha Kiswahili ukitaja tungamo ya takribani gramu 28. Unafanana na kipimo cha kizungu cha aunsi (ing. ounce). Wakia wa dhahabu wa Kiingereza hufafanuliwa siku hizi kuwa gramu 31.1034768.

Waswahili wa zamani walipokea kipimo hiki kutoka lugha ya Kiarabu. Katika nchi za Kiislamu wakia ilikuwa sehemu ya 12 ya "ratl" (ratili) lakini ilhali jina la "ratili" iliweza kutaja uzani tofauti sana kati ya gramu 340 hadi kilogramu mbiloi, hata wakia zilitofautiana.[1] Wakia iliyotumiwa katika Afrika ya Mashariki ilifanana na wakia. Matumizi yake ilisanifishwa kwa kutumia sarafu ya reale kama uzani sanifu.

Wakia wa kisasa

Wakia wa kisasa pia huitwa aunsi. Hufafanuliwa kuwa gramu 28.349523125, au 1/16 ya ratili.

Tanbihi

  1. Wehr-Cowan wanataja waqiya ya Misri kuwa gramu 37, ya Beirut 213.39, ya Yerusalemu 240, uk 1095

Marejeo

  • Wehr, Hans ed J M.Cowan (1976). A dictionary of modern written Arabic. Wiesbaden - New York: Spoken Language Services Inc. ISBN 0-87950-001-8